al-Sisi asema hatozungumza na Trump kuhusu mpango wa Gaza
12 Februari 2025Kulingana na vyanzo vya Misri, iliwekwa wazi kwa waziri wa mambo ya nje wa Misri Badr Ahmed Mohamed Abdelatty wakati wa mkutano na mwenzake wa Marekani Marco Rubio kwamba mpango wa kuwahamisha wakazi wa Gaza ulikuwa katika ajenda ya mkutano huo katika ikulu ya White House ikiwa Rais Al sisi angefanya ziara nchini humo.
Usitishaji mapigano Gaza hatihati
Vyanzo hivyo vimeongeza kuwa Abdelatty alijibu kwamba mkutano kama huo haungekuwa na tija na kwamba majadiliano yoyote yangepaswa kuwa juu ya mpango wa Misri katika ujenzi wa Gaza.
Misri na Qatar zawasiliana na Marekani
Chanzo kilichozungumzia na shirika la habari la AFP kwa sharti la kutotambulishwa, kimesema kwamba Misri na Qatar zinazosimamia mazungumzo ya amani yaGaza zinawasiliana na upande wa Marekani.
Chanzo hicho kimeongeza kuwa wapatanishi hao wanajizatiti kutatua mgogoro huo na kuilazimisha Israel kuzingatia hatua za kibinadamu katika makubaliano ya kusitisha mapigano, pamoja na kuanza mazungumzo ya awamu ya pili.
Makubaliano ya amani kwa Gaza yako chini ya shinikizo
Katika siku za hivi karibuni, makubaliano hayo ya amani yanayoendelea, yamekabiliwa na shinikizo baada ya waziri mkuu waIsraelBenjamin Netanyahu jana kuonya kwamba mapigano yanaweza kuanza tena ikiwa mateka wa Israel hawataachiliwa huru kufikia Jumamosi.
Tishio lake ni sawa na lile lililotolewa na Trump siku moja kabla ambapo alisema kuwa hali itakuwa mbaya ikiwa Hamas itashindwa kuwaachilia mateka wote wa Israel ifikapo Jumamosi.
Hamas yaipongeza Jordan na Misri kwa kumpinga Trump
Kundi la Hamas limepongeza hatua ya Jordan na Misri ya kupinga mpango huo wa Trump na kwa kuthibitisha kuwa kuna mpango wa mataifa ya Kiarabu ya kuijenga upya Gaza bila ya kuwahamisha wakazi wake.
Vyombo vya habari vya Korea Kaskazini vyaishtumu Marekani
Vyombo vya habari vya serikali ya Korea Kaskazini leo vimeishtumu Marekani kutokana na mpango uliopendekezwa wa kuijenga upya Gaza kwa kuchukua eneo hilo lililoharibiwa na vita na kuwahamisha wakazi wake mahali pengine.
Netanyahu atishia kuanza mapigano tena Gaza
Bila ya kumtaja moja kwa moja Trump, shirika la habari la KCNA kupitia tovuti yake ya Kiingereza, limeripoti kuwa ulimwengu kwasasa umeghadhabishwa na tamko hilo la Trump.
Ujerumani kupeleka vikosi vya polisi kwa ujumbe wa EU Rafah
Baraza la mawaziri la Ujerumani, limeamua kimsingi kupeleka vikosi vya polisi katika ujumbe wa kiraia wa Umoja wa Ulaya kusimamia kivukio cha mpakani cha Rafah kati ya Gaza na Misri. Haya yamesemwa na chanzo kimoja kilicholiarifu shirika la habari la Reuters.
Chanzo hicho kimeongeza kuwa muda halisi pamoja na ukubwa wa mchango wa Ujerumani ili kuhakikisha usalama wa eneo hilo muhimu la kuingia na kutoka Gaza bado havijaamuliwa.