MigogoroKenya
Al Shabaab yawaua maafisa sita wa polisi nchini Kenya
23 Machi 2025Matangazo
Taarifa ya polisi imesema wanamgambo wa al-Shabaab wa Somalia wenye mafungamano na kundi la kigaidi la al-Qaeda ndio wanashukiwa kwa mauwaji hayo.
Washambuliaji kutoka kundi hilo walianzisha mashambulizi alfajiri katika kambi inayowahifadhi askari wa akiba na walitumia silaha za aina mbalimbali kuivamia kambi hiyo.
Siku ya Jumanne ubalozi wa Marekani ulitoa tahadhari kwa Wamarekani ya kutosafiri kwenda katika baadhi ya maeneo nchini Kenya ikiwemo Garissa na kaunti zingine kwenye mpaka na Somalia kutokana na vitisho vya ugaidi.