Afisa wa polisi Kenya akamatwa kwa mauaji ya Albert Ojwang
13 Juni 2025Matangazo
Msemaji wa polisi Michael Muchiri, amelithibitishia shirika la habari la AFP kwamba afisa huyo wa cheo cha konstabo tayari ametiwa nguvuni.
Hata hivyo hakutoa maelezo zaidi na kuelekeza maswali yote kwa Mamlaka Huru ya Uangalizi wa polisi IPOA.
Waandamanaji watishia kutatiza shughuli ya bajeti Kenya
Wakati huo huo, msemaji wa IPOA inayochunguza kifo hicho, hakujibu mara moja ombi la tamko kutoka kwa AFP kuhusiana na kisa hicho.
Awali, polisi ilikuwa imesema kuwa Ojwangalifariki baada ya kujigonga ukutani, lakini baadaye, mwanapatholojia wa serikali alitoa ripoti iliyokinzani na taarifa hiyo.